Na Mustafa H. Piku Malibiche
Karibuni wasomaji wetu katika somo la Kiswahili. Leo tutatoa ufafanuzi wa maswali mawili ambayo ni:
MASWALI:
1.
Kwa kutumia jedwal la sauti IPA, kueleza
dhana ya ughuni na sighuna ukihusisha mahali na jinsi ya matamshi ya konsonanti
zisizopungua kumi.
2.
Kwa kutumia mifano mbalimbali, eleza
mbinu mbalimbali zinazoweza kutumika kuunda maneno ya lugha. Mifano iwe ya kitabuni
na isiyo ya kitabuni.
SWALI LA I -MAJIBU
Majibu ya swali hili yamegawanyika
katika sehemu kuu tatu ambazo ni utangulizi unaoelezea maana ya jedwali la
sauti (IPA), maana ya dhana ya ughuni na si ghuna na konsonanti.Sehemu ya pili
ni kuhusisha ughuni na sighuni na mahali na jinsi ya matamshi ya konsonanti na
mwisho ni hitimisho.
Jedwali la herufi za
konsonanti (IPA) linaelezea mahali pa matamshi, jinsi matamshi yanavyofanyika
na hali ya ughuna au si ghuna wa konsonanti husika (Roach, 1997, Uk.19).
Ughuni
unaelezewa kuwa ni hali ya utoaji wa sauti inayotokana na mtetemo wakati wa
matamshi ya herufi za konsonanti, utamkaji ambao husababishwa na hewa itokayo
kwenye mapafu kubanwa na ala za sauti kuachiwa na kusababisha mtetemo wakati wa
kutamka baadhi ya sauti. Si-ghuna inaelezwa
kuwa ni uhafifu wa sauti za herufi za konsonanti unaosababishwa na kuzuiwa na
kuachiwa ghafla kwa hewa wakati wa utamkaji wa baadhi ya konsonanti na hivyo
kutokuwa na mtetemo wa ala za sauti (Roach, 1997, Uk 31)
Konsonanti ni foni au herufi
ambazo wakati wa kutamka kwake hewa hutatizwa kwa namna fulani, wakati mwingine
hewa huzuiwa na wakati mwingine hutatizwa kiasi au kubanwa kiasi baada ya
kupitia koromeo.
Uainishwaji wa
Konsonanti katika jedwali la IPA unathibitisha aina kuu sita za sifa za
konsonanti kwa makundi kama ilivyoelezwa
na Masamba na wenzake (2006) na Mgulu (1999) na Taasisi ya Ukuzaji
mitaala Tanzania (1992, Uk. 63) kama ifuatavyo: vizuiwa/vipasuo, vikwamizi,
vizuiwa-kwamizi, vimadende, nazali (ving’ong’o) na Vitambaza.
Vipasuo (vizuiwa) ni
konsonanti ambazo hutokea wakati hewa ya mapafuni hupitia chemba ya mdomo na
kubanwa kabisa na kuachiwa ghafla na kusababisha mlipuko unaosababisha utokeaji
wa sauti hafifu na zenye mtetemo. Vipasuo ghuna ni [p] hutokea baada ya kukutana
kwa midomo yote miwili, [d] hutokea wakati ncha ya ulimi inapokutana na ufizi
wa juu, [g] hutokea baina ya kiganja cha ulimi kinavyokutana na kaakaa laini
ambavyo uhusishwa na kubanwa kwa hewa na kuachiwa kwa ghafla na kusababisha
utokeaji wa mrindimo wa sauti (nyuzi za
sauti).
Nyongeza ya hapo pia
kuna vizuiwa ambavyo ni si-ghuna ambavyo ni [p] ambayo hutokea baadaya midomo
miwili kuzuia hewa itokayo mapafuni na
kuachia mpenyo ghafla na kuruhusu mpasuko wa hewa, [t] ambayo hutokea baina ya
ufizi na ncha ya ulimi, na [k] ambayo kinachotokea baina ya sehemu ya nyuma ya
ulimi inapokwamiza hewa katika kaakaa
laini na kuachia hewa kwa ukakasi.
Vikwamizi, hutokana na
kukwamizwa kwa hewa na ulimi katika kaakaa gumu. Sauti hizi hutamkwa pale
ambapo ala za matamshi huwa zinakaribiana na kusababisha hewa inayopita toka
mapafuni kukwaruza ala za sauti. Vikwamizi hivyo ni [v], [z], [j], ambavyo ni
ghuna na [Ѳ], [f], [s], [ᵭ] na [h] ambavyo ni so-ghuna. Vikwamizi ghuna [v]
hutokea wakati midomo ya chini inapokutana na meno ya juu, [z] hutokea wakati
ala sogezi ya ulimi inaposogelea katika ufizi na kusabaisha kukwamizwa kwa hewa
na kuzaa sauti mtetemo, na [j] hutokea wakati sehemu ya juu ya ulimi
inaposogelea kaakaa gumu na kukwamiza hewa itokayo mapafuni.
Nyongeza ya hapo ni
kwamba; Vikwamizi so ghuna kwa mfano [f]
hutokea wakati midomo ya chini inaposogeleana na meno ya juu na kukwamiza hewa
itokayo mapafuni na hewa hiyo kuachiwa ghafla , [s] hutokea kwenye ufizi
kutokana na hewa kutoka mapafuni kuruhusiwa kutoka nje wakati ulimi umerudi
nyuma na kuachia mwanya wa hewa kupita, [ᵭ] hutokea kwenye meno yanapo na ulimi
na kusababisha hewa itokayo mapafuni kukwamizwa na ikiachiwa huku ikitetema na
kutoa sauti n.k.


Kimadende ni sifa ya
konsonanti ambayo hutokea inayotokea wakati wa kupigwapigwa kwa ulimi kwenye
ufizi. konsonanti [r] ni ghuna mfano wa sauti ya neno /refu/.
Nazali (ving’ong’o)
navyo vyaweza kuwa ghuna na so ghuna.Mfano wa sauti hizo ni [m], [n], na
[ŋ].Konsonanti hizo hutokea kwa kuhusishwa kimio na na hewa kutoka mapafuni
huelekezwa kupitia chemba ya pua ambapo hewa huzuiwa katika sehemu mbalimbali
za chemba ya kinywa na kuruhusu ipitie katika chemba ya pua. Herufi [m] ni
ghuna inayohusisha hewa kuzuiwa na mdomo, [n] ni ghuna inayohusisha hewa
kuzuiwa na ulimi, [ŋ] inayohusisha hewa kuzuiwa kwenye kaakaa laini.
Vitambaza ni konsonanti
ambayo ni kitambaza [l] ambayo ni ghuna inayotokea wakati sehemu ya kati ya
ulimi inapogusana na kaakaa gumu na
kuacha nafasi ndogo ya hewa kupita ikisababisha mkwaruzo ambao si mkubwa sana.
Hewa hiyo husukumwa nje, kuzuiwa na kuruhusiwa kupita pembeni mwa kizuizi
ambacho ni ulimi.
Tunaweza kuhitimisha
kuwa b, d, g, j, l, m, n, r. na t ni herufi ambazo zimeelezewa katika dhana ya
ughuni na p, f, k, na t katika dhana ya si-ghuni kama ilivyoelezwa katika
jedwali la IPA namna ambavyo sauti hizo hutokea.
REJEA
1. Massamba,
D.P.B., Y.M. Kihore na Y.P. Msanjila (2004). Fonolojia ya Kiswahili Sanifu
(FOKISA):
Sekondari na Vyuo, Dar es Salaam,
Taasisi ya Uchunguzi wa
Kiswahili, Chuo Kikuu
cha Dar es Salaam
2.
Mgullu, R.S. (1999). Mtaala wa Isimu: Fonetiki na Fonolojia ya
Kiswahili. Nairobi:
Longhorn Publishers.
3.
Roach, P.(1997). English Phonetics and Phonology. Second Edition- A self-Contained
Comprehensive
Pronunciation Course. Cambridge University Press.
4. Maganga.C,
Mbunda. F.L., na wenzake (1993).Kiswahili Vyuoni. Taasisi ya Ukuzaji Mitaala
Tanzania.KIUTA-NPC-Dar
es Salaam
Kuundwa kwa maneno ya
lugha ni dhana ya inayoashiria kukua kwa msamiati na matumizi ya lugha hiyo.
Kwa maana nyingine, ni kupanuka kwa matumizi ya lugha. Mbinu rahisi inayotumika
katika kuunda maneno ya Lugha ya Kiswahili ni pamoja na kukopa maneno toka
lugha nyingine mfano; Kiswahili kukopa baadhi ya maneno kutoka kiarabu kama
vile neno alasiri ( adhuhuri)
Zipo kanuni nyingi za
uundaji wa maneno katika lugha. Baadhi ya njia/ mbinu zitumikazo katika uundaji
wa maneno ya lugha ya Kiswahili ni: Uambishaji na unyumbuaji, uambatishaji,
urudufishaji, akronimi na uhulutishaji na uundaji mpya wa maneno.
Uambishaji wa maneno unamaanisha
ni tendo la kunyumbua baadhi ya maneno ya Kiswahili kwa kuambisha mofimu tangulizi
na au mofimu fuatishi za neno hilo na hupewa maana tofauti na aghalabu
huingizwa kwenye kundi tofauti la
maneno, kwa mfano neno
Hoja: hoji, hojaji, hojiwa
Koma: Komesha, komoa
Vuta: Vutia, vutisha, vutika
Mizizi ya maneno hayo
yaweza kuwekewa mofimu tangulizi na mofimu fuatishi na kupata majina mengine
toka katika neon la awali mfano:
Gomb- gombana, gombanisha, ugomvi,
mgombezi, magombano.
Njia ya pili ni
uambatishaji. Njia hii uhusika na uwekaji pamoja wa maneno mawili au zaidi ili
kuunda au kuzalisha neon jipya. Njia hii ni namna nyingine ya unyambulishaji.
Mwambatishaji maneno, badala ya kunyambua mofimu katika mzizi, huweka maneno
mawili au zaidi pamoja. Maneno haya yanaweza kuwa huru au kuambatishwa na
kunyambulishwa na mofimu. Kwa mfano;







Uambataji
huu wa maneno huunda/huibua fasili ya upamoja wa neon linalopatikana. Hii ina
maanisha kuwa kwa mfano fasili ya askari+ kanzu pekee hupoteza uhusiano wa
maana ya askari kanzu. Maana ya kila neno pekee hutofautiana katika neon
lililoundwa.
Njia
ya tatu ni urudufishaji.Katika njia hii, uundaji wa maneno hufanywa kwa urudufu
ambapo maneno au sehemu ya neno hurudiwarudiwa. Urudufishaji wa neon zima ni
urufishaji kamili na urudufu sehemu ya neon huitwa nusu rudufu. Kwa mfano:
-bara+bara=barabara
-nungu+nungu=Nungunungu
-Ki+wili-wili=kiwiliwili
-Ki+nyevu+nyevu= kinyevunyevu
Katika
uundaji huu wa urudufu una msingi uliosawa. Maana ya neon moja hailingani na
maana ya maneno mawili yanayoletwa pamoja. Mfano:
-bara- nchi kavu
-barabara- haimaanishi nchi kavu bali
hubeba maana nyingine tofauti
-mbali na pwani
-pande mojawapo ya
nchi kavu kumbe maana sahihi ni ya njia ndefu au njia kuu.
Njia/mbinu
ya nne ni Akronimi na uhulutishaji. Njia hii hufupisha maneno yanayotumiwa kwa
pamoja kwa kuchukua herufi za mwanzo tu maneno hayo mfano kutoka lugha ya
kiingereza ni neno “NATO-North Atlantic Treaty Organization”. Katika lugha ya
Kiswahili maneno kama:
-UKIMWI-Upungufu wa Kinga Mwilini
-TUKI-Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili
-BAKWATA-Baraza la Kuu la Waislamu
Tanzania
-BAKITA- Baraza la Kiswahili la Taifa
-BAWATA-Baraza la Wazee Tanzania
-MKUZA-Mkakati wa Kupunguza Umaskini
Zanzibar
Tendo
hili huitwa Akronimi. Tendo jingine linalofanana na hili ni uhulutishaji
(blending). Ni tendo linaloweka pamoja baadhi ya vijisehemu vya maneno ili
kuunda neno jipya. Mfano:
-Chakula cha jioni- chajio
-Hati za kukataza- Hataza
-Hati za kupunguza-hakuza
Njia
ya tano ni uundaji wa maneno mapya. Njia hii uhusisha mawazo mapya na kupewa majinaili kuleta dhana fulani mpya.
Utaratibu wake huanza kuchunguzwa uasili
wa lugha za asili kuona maneno yabebayo dhana husika. Mfano:
a.
Ngeli: (Kihaya) likimaanisha aina ya
vitu kuonesha majina
b.
Ikulu: (Kinyamwezi)-likimaanisha
maskani/ nafasi ya mkuu wa nchi/ temi za wanyamwezi
c.
Beberu: Dume la mbuzi (maana ya asili),
mtu aaminiye na kutetea siasa za ubeberu (utumiaji wa nguvu)-maana mpya.
Neno
likikosa uasili toka katika makabila, huangaliwa lugha nyingine za kigeni na
kurekebishwa kifonolojia na kimofolojia ili yaafikiane na kanuni za lugha ya
Kiswahili kwa kuzingatia kanuni za mfuatano wa fonimu kwa mfano:
KIKI- Konsonanti, irabu, konsonanti,
irabu
KIIKI- Konsonanti, irabu, irabu,
konsonanti, irabu
KIKKI- Konsonanti, irabu, konsonanti,
konsonanti, irabu. Mfano ”shirt”-shati, “bicycle”-
Baiskeli, “bible” –biblia
Endapo
inatokea neno la lugha nyingine kukosekana kupatikana basi neno jipya huundwa.
Mfano: Ukarabati, Ukarafati, Kongamano, warsha.Uuundaji wa maneno huzingatia
kanuni mbalimbali mfano, uambishaji na unyambuaji kama vile soma-
m-som-i,u-som-i.Mchezo-m-chez-o, m-chez-aji.
Ili
kuhitimisha, Njia hizi zote zimeelezwa kuwa na taratibu za kisayansi ya lugha
ambazo hufuatwa ili kuleta ulinganisho na upatanisho wa kisarufi wa maneno
husika ambayo huzaa sentensi.Hivyo basi uundwaji wa maneno hutumia njia nyingi
kati ya hizo zilizotajwa ambazo ni
REJEA
Maganga.C.,Mbunda.
F.L., na wenzake (1993).Kiswahili Vyuoni. Taasisi ya Ukuzaji Mitaala
Tanzania.KIUTA-NPC-Dar es
Salaam
Comments
Post a Comment